Tuesday, March 3, 2020

LIACHE CHOZI LANGU : Sehemu ya 1



SEHEMU YA KWANZA
WATUNZI WASTARA JUMA &@hadithizetu
WHATSAPP 0769510060
Matatizo tumeumbiwa binadamu, mda mwingine wengi ukata tamaa kabisa kwa fikra za kwamba wao ndio wenye manyanyaso na mateso tu, lakini chukua mda kaa hata barabarani, kisha uliza watu kumi tu, ambao ni wapita njia matatizo yanayo wazunguka, utaona yako madogo, unaweza kuwa mpole mwenye tabasamu lako lifichalo matatizo yanayo kuumiza lakini binadamu wanaweza kukuumiza kwa maneno, masekenyo na hata kutamani ufe ili iwe furaha kwao. Wasingekuwa binadamu mpaka sasa familia yangu ingekuwa na maendeleo, amani, furaha na yenye baraka lakini nakumbuka na siwezi kusahau kabisa, kuna siku moja nikiwa nyumbani namuandalia Frank chakula cha jioni, maana ndio alikuwa chaguo la moyo wangu na nilimpenda mpaka akanioa nikaanza kuishi nae pamoja, lakini siku hiyo jioni mme wangu alikuja akiwa amenuna sana, “Frank mme wangu tatizo nini,mbona leo huna furaha”, “Wastara nimechoka kuishi hivi, hivi unazani huko nje nachukuliwaje, yaani mda wote huo tuko pamoja, hata kupata kichefuchefu sijawai ona, naomba uchukue vitu vyako urudi kwenu, nimeisha choka kusemwa na ndugu” alijibu mme wangu akiwa na hasira sana, “hapana Frank usichukue maamuzi hayo, mtoto ni majaaliwa, naamini tutampata mtoto mme wangu, usisikilize maneno ya watu kwenye mahusiano yako, hayajengi mme wangu, yanabomoa tu” nilimjibu frank nikiwa katika sura ya uzuni sana.
Mme wangu alianza kubadilika, akija nyumbani anahakikisha ameisha lewa, kutokana na zile pombe basi akawa anaongea maneno ambayo yalikuwa yanautesa sana moyo wangu, hata huduma ya chumbani akaanza kunibania, kila nilipo onyesha kunyenyekea ili akae sawa lakini ni majibu mabaya tu nilikuwa nayapata, “hivi wewe mwanamke mbona unashobo sana, kwani wanaume wapo wangapi duniani, mimi kweli nimekuchoka Wastara naomba tu uondoke, siutafute mwanaume ambae hana uwezo wa kuwa na mtoto kama wewe ili muishi hivyohivyo” alisema Frank bila hata huruma lakini kwasababu nilikuwa nampenda nilipambana sana nikaendelea kuwa king’ang’anizi kwake.
Siku moja nikiwa nafaya usafi chumba nilicho kuwa nalala na mme wangu, kumbe Frank alienda kuninywea pombe za asubuhi kumbe baa aliyo kuwepo kulikuwa na mdada mmoja ambae alikuwa anauza hapohapo pombe, sasa kwasababu ya ulevi wa mme wangu bila hata aibu akapendana na yule dada na akamwambia aje anipige kisha mimi nichukie ili niondoke alafu frank aishi na yule Lucy pale nyumbani. Kweli wakati nafanya usafi nilishangaa kuona yule dada alie kuwa amevaa sketi fupi sana yenye kumshawishi mwanaume yoyote mwenye tamaa anaingia ndani, “dada naomba upishe kwa mme wangu”,alisema Lucy, “nikupishe kwangu, nikupishe wewe kama nani”, “kwataarifa yako umechokwa dada ehh, mtu gani uzai, mme wako yupo hapo nje kaongee nae, kwa jina naitwa Lucy alafu waga siongeagi sana, nimemaliza , kwa msaada zaidi labda uwe msaidizi wangu wa kazi humu ndani” alisema Lucy akiwa anabinuabinua macho, hasira zilinipanda machozi yakinitoka, nilimshika shingo yule dada, kisha nikamdondosha kitandani, “nakufaaa nauliwaaa ndani, njoo unisaidie mme wangu” alisema Lucy, hapohao frank akaja, “huyo Malaya wako ameniumiza angalia alivyo nitoboa na kucha”, Frank alichukia sana, alinizaba kofi ambalo sitalisahau maisha yangu yote, kipindi bado nimezubaa akanipiga mtama (ngwara) nilijigonga kichwa chini mpaka damu zikaanza kutoka puani,na niliogopa zaidi maana hata mdomoni pia damu zilikuwa zinanitoka, “mpuuzi sana, unampiga huyu mwanamke unamfahamu,” alisema Frank kisha akachukua nguo zangu tu na kuzirusha nje, akasahau kabisa kipindi ananileta kwake hakuwa hata na kitanda na hata vyombo vya ndani nilikuwa najibana hela kidogokidogo kisha nanunua, lakini nikapewa nguo tu,hata viatu vyangu hakunipa.
Nilitoka nje nikaanza kulia kisha nikarudi ndani nikisema “nisamehe mme wangu nipo tayari kuwa mke wako wa pili, naomba unisaidie” lakini walivyo na roho mbaya bila hata huruma walivuana nguo zao na kufanya tendo mbele ya macho yangu, kile kitendo kiliniuma sana ikabidi nirudi kukaa nje ya mlango, na kwadhalau yule dada akaanza kujitolesha sauti ili nijue bado wanaendelea kufanya lile tendo, “endelea mume wangu, nakupenda bby ohhhshhh” hizi sauti zilijirudia kutoka kwa Lucy, niliumia sana pale nje, nikatamani hata kuua, nikaona itakuwa dhambi, wazo likasema bora nijiue lakini nikaogopa maana nilitamani kuishi,ndipo wazo zuri la busara likaniijia kwamba, “kumbuka mme wako amelewa subiri amalize kufanya uchafu wake huenda atakusamehe” nilisubilia pale nje kwa mda mrefu, mpaka mvua ikaanza kunyesha, “Frank mme wangu naomba unifungulie nanyeshewa huku nje”, “nani mme wako, ondoka mimi sikujui”
Niliamua kukusanya nguo zangu zikiwa zimelowa, huku na mimi pia nimenyeshewa,kisha nikaanza kutembea ili nirudi nyumbani, umbali ulikuwa mrefu na kibaya zaidi Frank hakunipa hata mia,na hela yangu iliyo kuwa kwenye kibubu chini ya kitanda sikuweza kuichukua maana nilisukumwa nje na sikuweza kuingia tena ndani, kutokana na umbali wa mpaka kufika kwetu nilifika sehemu ikabidi nipumzike na ubaya zaidi kulikuwa na kigiza, kumbe pembeni kulikuwa na vijana wanacheza kamali, huku wanavuta Bangi, kuna mmoja aliniona akawaita wenzake, walikuja pale, “wewe mdada unajiamini vipi kukaa masikani kwetu mpaka mda huu”,”naombeni mnisamehe, nimepata matatizo mme wangu kanifukuza nipo naelekea kwetu lakini nimechoka ndio maana nimepumzika hapa”, “basi hamna shida, naamini utakuwa umechoka njoo hapo pembeni tukupe japo maji”, nilifurahi nikawaona wema sana, nilipo fika pembeni nikasikia kwamba, “vua nguo haraka tukupe maji yako”, nikaanza kushika begi langu ili wasije kuninyang’anya, “haaaaa, haaa ,haaa, unatubishia” walisema wale vijana maana walikuwa nane, mmoja akachomoa kisu, nikaona kuliko kufa bora niachie, kweli walinivua, kisha wakanichangia wote kimwili, nilipatwa na maumivu, kibaya zaidi wakaweka nguo yangu ya ndani mdomoni na kitambaa nilikuwa nacho eti nisipige kelele, maumivu niliyo yapata pale sikuwai kuyapata tangu nazaliwa walinifanya niumie sana sehemu yangu ya siri, niliishiwa hata nguvu mpaka nikapoteza fahamu, nilikuja kushtuka usiku nguo zangu zote zimechukuliwa nikiwa nimebaki na kitambaa pamoja na nguo yangu ya ndani mdomoni, niliivaa ile nguo kisha nikaanza kushindwa naendaje nyumbani, kipindi kunaanza kukucha kuna wakaka wawili walikuwa wanapita, moyo ulikataa kabisa kuwaita lakini niliogopa jamii itanichukuliaje mchana nikionekana uchi, hivyo nikataka kuwaomba msaada wakunitafutia nguo,niliwaita wakaja, mmoja wao akasema, “kaka hii ndio mikosi, huyu atakuwa mshirikina, ameanguka na ungo hapa, anatakiwa kufa tuwaite binadamu wamuue”, mwenzake akajibu, “hapana kaka, tazama dada wawatu analia, tungemuuliza kwanza anatatizo gani” niliwaelezea nilivyo bakwa ndipo mmoja wao akanifatia nguo kisha wakanisaidia hela ya nauli, alie nipa hela alikuwa anaitwa, Mussa, na mwingine Samweli, nilienda mpaka nyumbani nikiwa na maumivu sana, wakati nakaribia na mazingira ya nyumbani nikashangaa sana kukuta wanakijiji wengi pale, nilipo sogea kwa mbele nikakuta wengine wanalia, ndipo nikauliza kuna nini watu wakaanza kulia sana, kumbe mama pamoja na mama yangu wote walikuwa wamefariki na kibaya zaidi ndani ya siku moja…
USIKOSE EPISODE YA PILI
LIACHE CHOZI LANGU
IMEANDIKWA NA WASTARA JUMA PAMOJA NA @hadithizetu
Whatsapp +255769510060

Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only